Saturday, November 17, 2012

MWALIMU MWENYE UKWELI HALISI


WASIFU WA MWALIMU

        Tangazo la biashara: Ahadi kwamba atapunguza kilo 11 katika majuma mawili kwa kutumia kitu kilichokuwa kinatangazwa.
       Chumvi nyingi ilikuwa imeongezwa: alipunguza siyo zaidi ya nusu kilo.
        Watabiri wa hali ya hewa walitangaza kuwa kesho yake ingekuwa siku ya jua na joto mwisho wa mwezi wa nne (Aprili).
       Pilipili ilikuwa imeongezwa: kesho yake kukawa na mawingu, radi na mvua kubwa ya mawe.
        Yule jamaa aliyekuja kukuuzia ile simu pale kwenye stendi ya basi; alikuuzia kwa nusu ya bei halisi ya ile simu.
       Huyu alikuwa amechanganya chumvi na pilipili na chloroquine: Alikuwa ameiiba simu hiyo kwa abiria mwingine kama wewe muda mfupi kabla. 
              
Hivyo ndivyo sifa za watu zinavyotangazwa na kuwekwa mbele za jamii ya wakazi wa dunia. Kuna chumvi nyingi, pilipili na hata sumu zinazochanganywa ndani yake. Ukweli wenyewe hauelezwi, na uongo mwingi hutangulizwa!
        Wengi wanasemwa katika hali ambayo si ya kweli (too good to be true)! Na bado ulimwengu unanunua taarifa hizo na kuzishangilia.
        Mwalimu wa kweli hatangazwi na kile watu wasemacho kumhusu, bali kwa yale aliyoyatenda, anayoyatenda na atakayotatenda! Wasifu wake unajiuza; “chema chajiuza, kibaya chajitembeza”
        Mwalimu Mwenye Ukweli Halisi anajiuza kwa kazi zake za thamani kuu!!!

WASIFU WA MWALIMU
        JE, YEYE ALIKUWA NANI?
        YEYE NI NANI?
        ALIFANYA NINI?
        ANAFANYA NINI?
        ATAFANYA NINI?
        WASIFU WAKE UNAKUHUSUJE?

        YEYE ALIKUWA NANI NA NI NANI SASA?
      Yohana 1:1-3, 14 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu. Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika….     Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli.”
        1 Yohana 5:8: “Kwa maana wako watatu washuhudiao mbinguni, Baba, na Neno, na Roho Mtakatifu, na watatu hawa ni umoja.”

        ALIKUWAKO KWA MUNGU, NAYE ALIKUWA MUNGU:
         Yohana 8:58 “Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.”
        Waebrania 1:1,2 Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi, mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika Mwana, aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu.
        Mwanzo 1:26  “Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu…”
         Kumbukumbu la Torati 6:4 “Sikiza, Ee Israeli; Bwana, Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja.”
         Yohana 10:30 “Mimi na Baba tu umoja.” 

        CHEO “MWANA” KILIANZIA WAPI?